Updated News to your hands? Contact Us Join us!
Posts

Israel yashambulia kambi ya Wapalestina Jenin katika Ukingo wa Magharibi - Fastestsmm Swahili

Image caption: Sadio Mane na Yaya Toure

Yaya Toure anasema aliiomba Manchester City kumsajili Sadio Mane kutoka Southampton alipokuwa katika klabu hiyo.

Mshambulizi huyo wa Senegal alifunga mabao 21 katika mechi 67 za Premier League akiwa na Saints kuanzia 2014-2016 kabla ya kusajiliwa na Liverpool kwa £34m.

Aliendelea kuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Jurgen Klopp ambacho kilishinda Ligi ya Mabingwa 2019 na taji la kwanza la Ligi Kuu ya Reds mnamo 2019-20.

"Siku zote nilitaka kucheza naye [Mane]," Toure alisema.

Toure alikaa City kwa miaka minane kuanzia 2010-2018, akishinda taji la kwanza la Ligi Kuu na Kombe la FA.

Akizungumzia Mechi 10 Bora Afrika: kuhusu Mchezaji Bora wa Afrika Ligi Kuu ya Uingereza, kiungo huyo wa zamani wa Ivory Coast, 40, alisema: "Nilipokuwa City, wakati alipokuwa Southampton, nilimheshimu sana na alikuwa akiwauliza baadhi ya wakuu wangu wamsaini tu Lakini mwishowe haikufanyika.

"Baada ya hapo Klopp alikuwa na macho ya kumpata na sasa angalia alichokifanya kwa Liverpool, alikuwa na kipaji. Nampenda, nampenda kama mchezaji."

Mane alijiunga na Bayern Munich Juni 2022 kwa pauni milioni 35 baada ya kufunga mabao 120 katika michezo 269 na kushinda mataji sita makubwa Anfield.

Toure anasema nahodha huyo wa Senegal ni "mfano mkubwa" kwa kazi yake nje ya soka.

Mnamo Machi 2020 Mane alichangia pauni 41,000 kwa kamati yake ya kitaifa inayopigana dhidi ya coronavirus. Pia alitoa jezi 300 za Liverpool kabla ya Liverpool kupoteza fainali ya Ligi ya Mabingwa 2018 dhidi ya Real Madrid .

"Jinsi anavyoshughulika na mambo kwa urahisi na usaidizi anaoutoa kwa watu wake katika nchi yake ni wa ajabu, na kile ambacho amekuwa akihusika nacho," Toure aliongeza.

“Siku nyingine huwa nakasirika nikisoma vyombo vya habari kuhusu yeye na mwandishi wa habari akimuuliza mbona huna gari aina ya Ferrari na vitu, akasema, ‘Hapana, sihitaji, napendelea kuwa nayo gari la kawaida kuliko kuwa na Ferrari'.

"Miezi miwili baadaye tunamwona, amekuwa akifanya mambo katika nchi yake, ni mfano mkubwa."

[ad_2] #Israel #yashambulia #kambi #Wapalestina #Jenin #katika #Ukingo #Magharibi #Fastestsmm #Swahili https://fastest-smm.com/israel-yashambulia-kambi-ya-wapalestina-jenin-katika-ukingo-wa-magharibi-bbc-swahili-4/?feed_id=143516&_unique_id=64af4d7aef165
Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.